come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

TAIFA STARS KWENDA KAMPALA JUMATANO



Timu ya Taifa ya Tanzania itaondoka Mwanza Jumatano kwenda Kampala, Uganda kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la CHAN itakayochezwa Jumamosi katika Uwanja wa Mandela kuanzia saa kumi kamili jioni.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini jijini Mwanza chini ya Kocha Kim Poulsen tangu Julai 14 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
Timu hiyo itaondoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza saa 7.25 mchana kwa ndege ya PrecisionAir, na inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe saa 10.15 jioni.
Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya kikosi chake Jumanne.