come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

ARSENAL YAENDELEA KUMFUATILIA SEAREZ, WENGER ADAI ATANG'OKA TU


KLABU ya Arsenal imeendelea na harakati za kuwania saini ya mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez.
Arsene Wenger anaamini mchezaji huyo mwenye kipaji kutoka Uruguay ataisaidia Arsenal katika Ligi Kuu ya England na anataka kuvunja rekodi ya usajili ya klabu yake kwa kutoa Pauni Milioni 40.
Dau la Pauni Milioni 40 linaweza kuwa sawa kwa Suarez, lakini inafahamika Arsenal itatoa kwanza Pauni Milioni 35 na nyingine Milioni 7 saba watalipa kwa vipengele, maana yake hakuna namna ambayo Liverpool watakubali.
Fresh bid: Luis Suarez could yet leave Liverpool before the end of the season
Ofa ya mafungu: Luis Suarez yuko tayari kuondoka Liverpool kabla ya mwisho wa msimu
Ofa za awali za Pauni Milioni 30 na Milioni 35 tayari zimepigwa chini na Liverpool, ambayo ilimnunua kwa Pauni Milioni 22.7 Suarez Januari mwaka 2011, lakini Arsenal imemfanya mchezaji chaguo la kwanza katika inayowahitaji baada ya jithada zao za kumnasa Gonzalo Higuain kueleeka kukwama.
Rekodi ya Arsenal kusajili mchezaji kwa bei kubwa ni Januari mwaka 2009, ilipolipa Pauni Milioni 15 kumnunua Andrey Arshavin.