come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

CHELSEA BADO YAMTAKA ROONEY, YAPELEKA OFA NYINGINE

Departing? Wayne Rooney appears determined to leave Manchester United for ChelseaKLABU ya Chelsea iko tayari kutoa ofa ya pili ya kumsajili Wayne Rooney (Pichani). 

Kocha wa Stamford Bridge, Jose Mourinho bado anakaza masuli kumpata mshambuliaji wa Manchester United na ananiandaa kulipa Pauni 30 kukamilisha dili hilo. 
Chelsea iliwasilisha ofa ya awali wiki iliyopita, lakini ikakataliwa na klabu ya Old Trafford.

United ilikataa pofa ya Pauni Milioni 23 taslimu jumlisha Milioni 2.5 malipo ya ziada ikisistiza Rooney, mwenye umri wa miaka 27, hauzwi.
Chelsea inafurahi kumpa mshahara wa Pauni 240,000 Rooney kwa wiki anazolipwa United na watampa Mkataba wa miaka mitano kama atafanikiwa kulazimisha kuondoka kwa mabingwa hao wa England.
Rooney ambaye mambo yake hayajaeleweka anafanya mazoezi viwanja vya mazoezi vya United, Carrington baada ya kurejea kutoka kwenye kambi ya klabu kujiandaa na msimu kwa sababu ya kuumia nyama.
Ambitious: Jose Mourinho plans to bring Wayne Rooney to Chelsea
Matarajio: Jose Mourinho anataka kumsajili Wayne Rooney Chelsea
Pressure? David Moyes will be involved in his first title race
Wayne Rooney
Kipindi kigumu: Mustakabali tata wa Rooney unampa wakati mgumu David Moyes katika siku zake za mwanzo kazini United

Kocha wa United, David Moyes ameendelea kusistiza Rooney, ambaye amebakiza miaka miwili katika mkataba wake Old Trafford, hauzwi.
Lakini anaweza kupambana sana kumbakiza mchezaji huyo, kwqa sababu Mourinho anamtaka kweli Rooney na anapambana kumpata.