come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

Tonto aelezea filamu ‘Dirty Secret'

 
LICHA ya kuwa kinara wa kuvaa uhusika wa ukahaba na tabia zisizokubalika katika jamii bila kujali yanayosemwa na watu, safari hii mambo yamekuwa ni tofauti kwa mwigizaji, Tonto Dike.
Ameamua kuweka bayana sababu ya kukubali kuigiza filamu ya ‘Dirty Secret’ ambayo Tonto anaigiza kama msichana aliyekuwa na uhusiano wa kimapenzi na baba yake licha ya kuwa na mpenzi mwingine.
Nafasi ya baba katika filamu hiyo inaigizwa na Jibola Dabo aliyecheza kama baba mwenye mahusiano ya kimapenzi na binti yake. Nafasi ya mpenzi wa binti yake ikichezwa na Muna Obikwe.
Katika filamu hiyo mastaa hao watatu, kila mmoja alifanikiwa kucheza vizuri katika nafasi yake jambo lililochangia ujumbe kufika kwa usahihi.
Pamoja na ukweli huo, jamii ya Wanigeria ilikuwa na maswali mengi juu ya kwanini hasa mastaa hao waliamua kuigiza filamu hiyo wakidai haina uhusiano na utamaduni wa Wanigeria.
Katika mahojiano yake aliyoyafanya hivi karibuni, Tonto ameweka bayana sababu ya yeye kuigiza filamu hiyo akidai ni simulizi yenye maudhui ya kweli.
“Dirty Secret ni simulizi ya kweli kwani hata msichana aliyetokewa na mkasa huo nilikutana naye na ndio maana nikaguswa na kuicheza nafasi hiyo," alisema Tonto.