come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

BAYERN MUNICH NOMA, YAICHAKAZA KWA MATUTA CHELSEA

BAYERN Munich (Pichani) imetwaa Super Cup ya Ulaya baada ya kuifuna Chelsea kwa penalti 5-4 kufuatia sare ya 2-2 na Jose Mourinho ameshindwa kutwaa taji la kwanza baada ya kurejea darajani mbele ya Pep Guardiola.
Katika mchezo huo, ambao Chelsea ilimaliza pungufu baada ya Ramires kutolewa nje kwa nyekundu dakika ya 84, mabao ya The Blues yalifungwa na Torres dakika ya nane na Hazard dakika ya 93, wakati ya Bayern yalifungwa na Ribery dakika ya 47 na Javi Martinez dakika ya 120.
Katika mikwaju ya penalti, Ashley Cole alifunga Cech akaokoa penalti Xherdan Shaqiri. 
Penalti nyingine zilizofungwa na David Luiz, Oscar na Frank Lampard kwa upande wa  Chelsea, wakati za Bayern zilifungwa na Jerome Boateng, Toni Kroos, Philipp Lahm na Franck Ribery hivyo kuteneneza ushindi wa 5-4
Kikosi cha Bayern Munich kilikuwa: Neuer, Rafinha/Javi Martinez dk56, Dante, Boateng, Alaba, Muller/Gotze dk70, Lahm, Kroos, Ribery, Mandzukic na Robben/Shaqiri dk95.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Cahill, Luiz, Cole, Ramires, Lampard, Hazard, Oscar, Schurrle, Torres/Lukaku dk97