come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

NEYMAR ASEMA AMETUA BARCA KUMSAIDIA MESSI AENDELEE KUWA MCHEZAJI BORA DUNIANI

Arrival: Neymar was unveiled as a Barcelona player at the Nou Camp on MondayBAADA ya kukamilisha uhamisho wake kutua Barcelona, Neymar ambaye anaungana na Lionel Messi kuunda safu mpya kali ya ushambuliaji, ameweka wazi malengo yake.

Mbrazil huyo alisafiri moja kwa moja kwenda Hispania baada ya Brazil kutoa sare ya 2-2 nyumbani na England mjini Rio de Janeiro Jumapili, na katika mahojiano aliyofanyiwa kwenye Uwanja wa Nou Camp alisema: "Nipo tayari kumsaidia Messi kuendelea kuwa mchezaji bora duniani,".
 
Neymar alipokewa kifalme katika Uwanja wa Ndege wa Barcelona - kabla ya kupelekwa kwenye ofisi za klabu hiyo kwa ajili ya kupigwa picha akiwa na jezi ya Blaugrana kisha kwenda kufanyiwa vipimo vya afya.
 
Neymar alitambulishwa kuwa mchezaji mpya wa Barcelona Nou Camp jana
Mbrazil huyo amesaini Mkataba wa miaka mitano Catalan.
Dynamic duo: Neymar will join Lionel Messi in a formidable partnership for Barcelona
Neymar anaungana na 'mchawi' huyu Lionel Messi kuunda safu kali ya ushambuliaji Barcelona