come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

Super Nyamwela aja na staili mpya ya Bongo Pop

MNENGUAJI mkongwe wa bendi za muziki wa dansi nchini, Hassan Musa Mohamed maarufu kama Super Nyamwela anatarajia kuzindua staili yake mpya ya muziki itakayojulikana kama Bongo Pop.
Akizungumza na Mwananchi Nyamwela anayeshambulia jukwaa kupitia Bendi ya Muziki wa Dansi ya Extra Bongo, alisema hivi sasa amekamilisha wimbo mpya Dullee Duvellee ambao ameuimba kwa staili ya Bongo Pop.
“Hii ni staili mpya kabisa ya muziki hapa nchini, wimbo huu nimerekodi katika studio za C91 Records, zilizopo Kinondoni, nimemshirikisha msanii wa muziki wa kizazi kipya, Mukky kutoka katika Kundi la Makomandoo lililo chini ya uangalizi wa Tanzania House of Talent THT,” alisema Nyamwela.
Pia lisema baada ya kukamilisha wimbo huo mpya yupo katika mipango ya kuzindua staili yake mpya ya Bongo Pop.
‘’Staili mpya ya Bongo Pop, inakwenda na ‘Swaga za Duvellee Duvellee’ ambayo kwa Kiswahili cha mtaani ni Shwari Shwari, na tayari wimbo huu nimeusambaza katika vituo mbalimbali vya redio nchini na baadhi vimeanza kuutendea haki kwa kuupiga na kuwapa raha wasikilizaji,’’ alisema Nyamwela.
Pia Nyamwela amesema yupo katika maandalizi ya kurekodi video ya wimbo huo