come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

Yanga yailiza tena Simba

YANGA imewasainisha mastraika wawili. Mmoja wao ni Shabaan Kondo aliyefanya mazoezi siku tatu na Simba wiki iliyopita na imedai kwamba kwa kiwango alichonacho atachukua namba ya Mbwana Samatta ndani ya Taifa Stars.
Straika mwingine ametokea klabu ya Machava ya Moshi, Kilimanjaro inayoshiriki Daraja la Kwanza ambaye umri wake na kiwango chake ndiyo kigezo kilichombeba.
Kigogo mwenye ushawishi mkubwa kwenye usajili wa Yanga, aliuambia mtandao huu jana Jumatatu kwamba; "Tumesaini mastraika wawili, mmoja Kondo na mwingine anachezea Machava, ni vijana wadogo chini ya miaka 21, huyo Kondo tulimchomoa Simba alifanya nao mazoezi tangu Jumanne mpaka Alhamisi."
"Ni mchezaji mwenye mwili mzuri na uwezo mkubwa sana, tumemuona kwenye ligi ya Msumbiji na ninakuhakikishia ndiye straika ambaye anakuja kuchukua namba ya Samatta Taifa Stars, ngoja aanze kucheza utakubali maneno yangu. Yanga hatubahatishi safari hii, "alisisitiza kiongozi huyo.
Kondo alifanya mazoezi na Simba katika Uwanja wa Kinesi, Dar es Salaam kwa siku tatu wiki iliyopita, lakini 'akaibiwa' na viongozi wa Yanga.
Alisema kwamba picha nzima ya usajili wa Yanga itajulikana kabla ya wikiendi hii kwani Kocha Mkuu Ernest Brandts atakuwa amewasili kuendelea na progamu ya kuiandaa timu ambayo ilianza mazoezi mepesi jana Jumatatu chini ya Kocha Msaidizi Fred Minziro.
Kiongozi huyo alisema kwamba hawawezi kusajili wachezaji zaidi ya watano kwenye usajili huu kwavile timu yao ni imara na inahitaji mabadiliko madogo ya kujiimarisha tayari kwa Kombe la Kagame na Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani.
Wakati Yanga ikisajili wawili tayari Simba imeshasaini wachezaji zaidi ya 10  wa ndani baadhi yao wakiwa wale wa zamani walioongozewa mikataba na chipuzi ni wengi zaidi.