
Kocha wa Brazil , Luiz Felipe
Scolari, amesema kuwa mshambulizi nyota wa Barcelona ya Uhispania na
Brazil Neymar alikumbwa na mshtuko na kuhofia kuwa alikuwa amepooza
miguu yake punde baada ya kugongwa uti wa mgongo na kiungo wa Colombia
Juan Zúñiga .

Neymar alihofia kupooza
Kauli hiyo imemlazimi Scolari kupanga upya safu yake ya mashambulizi ilikufidia pengo aliyoiwacha Mshambulizi huyo machachari.

Picha za mshambulizi huyo akilia ziliwatamausha mashabiki wake kote duniani .

Neymar alipojeruhiwa na Juan Zuniga
Scolari amesema kuwa ''Bila shaka tumempoteza mchezaji ambaye anaweza kuleta tofauti kubwa mno katika mechi yeyote ile hususan katika mechi hiyo ya jumanne dhidi ya Ujerumani''