come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

TANZANIA HAIKUTUMA MAOMBI RASMI YA KUWA MWENYEJI WA AFCON 2017



Mpaka siku ya mwisho ya kupeleka maombi ya kuandaa michuano ya kombe la mataifa ya Afrika mwaka 2017 ni mataifa saba tu yaliyotuma maombi kuandaa michuano hiyo,hapo jana ililipotiwa ya kwamba Tanzania imetolewa kwenye mchakato huo wa maombi baada ya kuambiwa na CAF kuwa haina uwezo wa kuandaa hayo mashindano kwasasa,

Taarifa ambazo mtandao huu umezipata kutoka Makao makuu ya CAF jijini Cairo zinasema Tanzania haikupeleka maombi ya kuandaa mashindano hayo yanayotarajia kufanyika mwaka 2017.


Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya CAF mataifa yaliyotuma maombi rasmi kabla ya muda kufungwa hapo mnamo septemba 30,2014 ni Algeria, Egypt, Gabon, Ghana, Kenya, Sudan na Zimbabwe.

Maombi ya kuandaa mashindano hayo yalifunguliwa rasmi 23 August 2014, kufuatiwa kujiondoa kwa Libya,
Mwandaaji atakayepata nafasi atatangazwa na kamati ya utendaji ya CAF kupitia moja ya vikao vyake mnamo mwaka 2015.