come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

Ferdinand kulamba mwaka mmoja United

London, England. Rio Ferdinand anatarajia kusaini mkataba mpya na Manchester United wakati wowote kuanzia sasa, taarifa za ndani za klabu hiyo zilithibitisha jana.
Kocha mpya, David Moyes anatarajiwa kumpa mkataba wa mwaka mmoja baada ya ule wa kwanza kumalizika mwezi ujao. Tayari beki huyo ameshatangaza kuachana na soka la kimataifa ili aendelee kucheza Old Trafford.
Ferdinand amecheza mechi 33 msimu huu, zikiwemo 27 za Ligi Kuu ambazo ni nyingi kuliko beki mwingine yeyote wa nafasi ya kati na kuiwezesha Man United kutwaa ubingwa msimu huu. (BBC).