come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

CIRKOVIC AIPONDA SIMBA, ADAI INATESA MAKOCHA, AMSIFU BOBAN KUHAMIA COASTAL UNION

KOCHA wa zamani wa Simba, Milovan Cirkovic ameusifu uamuzi wa kiungo Haruna Moshi ‘Boban’ kuihama timu hiyo na kujiunga na Coastal Union.


Boban alisaini mkataba wa kujiunga na Coastal Jumapili ya wiki iliyopita baada ya uongozi wa klabu ya Simba kutoonyesha nia ya kumuhitaji tena.
Awali uongozi wa Simba ulimsimamisha Boban na wachezaji wengine saba wa timu hiyo baada ya kuwashutumu kuwa ni watovu wa ndhamu. Akizungumza na mtandao huu kwa njia ya simu jana, Circkovic alisema kuwa uamuzi wa Boban ni sahihi kwani utamwezesha kulinda kipaji chake kwani kilikuwa mbioni kupotea.
“Nimesikia Boban amehamia Coastal Union, ni uamuzi sahihi kabisa,”alisema kocha Circkovic.
Alisema,”Kama Simba wameonyesha hawamuhitaji ni bora ameondoka mapema kwa sababu hata kama atabaki hataweza kucheza hivyo itakuwa hasara kwa kipaji chake,” alisema Cirkovic.
Alisema anaamini tatizo linaloikabili Simba wakati huu ni chuki binafsi za baadhi ya viongozi wa Simba na siyo utovu wa nidhamu wa wachezaji.
Kocha Cirkovic aliwatahadharisha viongozi wa Simba kama wasipobadilika timu yao haitapata mafanikio. Pia, Cirkovic alipinga kitendo kilichofanywa na uongozi wa Simba cha kusitisha mkataba wa  kocha wa timu hiyo Patrick Liewig, akisema siyo suluhu ya kusaka mafanikio.