come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

MASIKINI!, BABI, UHURU WATEMWA AZAM


MASIKINI!,  Azam FC imewatoa kwa mkopo wa kwa heri kwa kiungo wake mkongwe Abdi Kassim ‘Babi’ na kumtema mshambuliaji wake Uhuru  Seleiman aliyekuwa kwa mkopo akitokea Simba SC.
 Meneja wa timu hiyo, Patrick Kahemela alisema  jana  kuwa sababu kubwa ya kuachana na  wachezaji hao ni mikataba yao kumalizika pamoja  na umri kuwatupa mikono.
Wachezaji waliotupia virago ni pamoja na Lewis  Cosmas aliyejiunga na Ruvu Shooting na Abdulhalim Humoud aliyepata timu Afrika Kusini  ya Jomo Cosmos.
Akizungumza na gazeti hili Abdi Kassim alisema “Ni  kweli mkataba wangu kuitumikia Azam umeisha  ingawa walinitaka nisaini mpya, lakini tukashindwa  kuafikiana. “Naamini bado nina nguvu na uwezo wa kucheza soka. Kwa hiyo niko tayari kujiunga na timu yoyote  ambayo itaonyesha nia ya kunitaka.” alisema Babi  aliyekipiga na klabu za Mlandege ya Zanzibar,  Mtibwa Sugar, Yanga, DT Long ya Vietnam  pamoja na timu ya Taifa ‘Taifa Stars’.
Anaeleza kuwa yuko tayari kujiunga na Yanga,  Mtibwa Sugar ama Coastal Union iwapo zitaonyesha kutaka kumsajili kwa ajili ya msimu ujao.
Klabu ya Mtibwa iliwahi kukiri kutaka kumrejesha  Babi nyumbani katika dirisha dogo la usajili  Januari mwaka huu.
Wachezaji wengine walioachwa na Azam ni kipa  Deogratius Munishi, Sunday Frank na Uhuru  Seleiman aliyekuwa akiitumikia klabu hiyo kwa  mkopo akitokea Simba.  “Munishi mkataba wake umekwisha  huku Uhuru  akirejeshwa Simba, baada ya kumaliza msimu wake  wa mkopo na Azam.” alisema Kahemela.
Alieleza kuwa kama ilivyokuwa wakati wa dirisha la uhamisho wa wachezaji msimu ulioisha Azam ilimsajili  George Odhiambo ‘Blackberry’ peke yake.
“Safari hii tena  tumeamua kuwapandisha wachezaji wawili wa U-20, Mudathir Yahaya na  kipa Hamadi Juma na kufunga zoezi la usajili,”
“Kwa mujibu wa ripoti ya kocha Stewart Hall, inaeleza hakuna sababu ya kwenda nje kusajili wachezaji ambao viwango vyao havipishani na waliopo klabuni.” alisema kiongozi huyo.
Aidha alisema wachezaji wengine wote waliosalia  wanabaki klabuni hapo ingawa,  kocha amependekeza baadhi ya vijana wa U-20 walioonyesha viwango vya juu wapandishwe timu  kubwa.
0
Share