come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

TFF yahofia usalama Simba, Yanga


SIMBA na Yanga hazitashiriki michuano ya Kombe la Kagame nchini Sudan,  iwapo Serikali itasisitiza amani iliyopo nchini humo siyo salama, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lilisema jana Dar es Salaam.
Kabla hata TFF haijatoa kauli hiyo kupitia kwa Mtendaji Mkuu, Angetile  Osiah, Serikali ilishatoa angalizo juu ya utata wa usalama nchini Sudan hasa  kwenye Mji wa Darfur ambako ni sehemu ya kituo cha michuano hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe  alisema bungeni wiki iliyopita wakati wa mjumuisho wa hotuba yake kuwa, Serikali haitakuwa tayari kuziruhusu timu zake kwenda kushiriki  mashindano hayo.
Jana, Osiah alisema TFF itatekeleza agizo la Serikali kuhusu hali ya  usalama, na kwamba Simba na Yanga ambao ni mabingwa wa taji hilo  hazitakwenda Sudan kinyume na agizo la Serikali.
“Kauli ya Membe ni muhimu. Serikali imejali usalama wa  watu wake,” alisema Osiah. “Tunaendelea kuwasiliana na Serikali kupitia ubalozi wetu Sudan kabla ya kutoa msimamo kutegemeana na tutakavyoelezwa. Kuna taarifa timu ya El-Merrheikh na Al-Hilal zimejitoa katika mashindano hayo kwa hofu ya usalama nchini humo.