come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

MBWANA SAMATTA AITIA PRESHA MOROCCO

MBWANA Samata na Thomas Ulimwengu wametuma salamu Morocco baada ya kuiongoza TP Mazembe kufuzu kwa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho.
TP Mazembe ilipokea kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Liga Muculmana ya Msumbiji, lakini wamesonga mbele kwa ushindi wa jumla 5-2.
Mshambuliaji Samata alifunga bao la kufutia machozi la Mazembe akiunganisha kwa kichwa kona ya Solomon Asante.
Hilo ni bao la tatu kwa Samata kufunga katika wiki moja baada ya kupachika mabao mawili waliposhinda 5-0 katika mechi ya Ligi Kuu DR Congo dhidi ya Molunge.
Katika mchezo huo wa ligi uliofanyika Kinshasa Jumanne iliyopita, Samata alifunga mabao mawili huku Ulimwengu na Given Singuluma, na Eric Bokanga kila mmoja akifunga bao moja.
Kasi ya Samata na Ulimwengu ilitosha kuisaidia Taifa Stars kuisambaratisha Morocco katika mchezo wa kusaka kufuzu kushiriki Kombe la Dunia 2014 uliofanyika mwezi Machi 24, ambapo Taifa Stars ilishinda kwa mabao 3-1.
Nyota hao wa TP Mazembe watajiunga na kambi ya Stars nchini Morocco tayari kwa mchezo wa marudiano utakaofanyika Jumamosi ijayo jijini Marrakech.
Wenyeji Morocco katika kuhakikisha hawapotezi mchezo huo, kocha wao Rachid Taoussi ameita kikosi cha wachezaji 24 kati yao 16 ni wale