come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

SIMBA YAZIDI KUMEGUKA, STRAIKA WAKE ABEBWA

Mshambuliaji wa Simba aliyekatisha mkataba wake, Abdalah Juma amesema msimu ujao ataichezea timu yoyote ya ligi daraja la kwanza na siyo Ligi Kuu tena.
Juma amesisitiza zipo timu nyingi zilizoonyesha kumhitaji kwa sasa, lakini ameamua kupumzika kucheza Ligi Kuu na msimu ujao atatafuta timu ya kuchezea katika ligi daraja la kwanza.
Akizungumza na mtandao huu jana, Juma alisema tayari amemalizana na uongozi wa Simba na kukabidhiwa barua ya maridhiano ya kukatisha mkataba.
“Nimemalizana na Simba na wakati wowote nitatangaza ni timu gani ya daraja la kwanza nitacheza msimu ujao,”alisema mshambuliaji huyo.