come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

WATOVU WA NIDHAMU SIMBA, WATOSWA ASHANTI

UONGOZI wa timu ya soka ya Ashanti United ya jijini Dar es Salaam, umesema kuwa haupo tayari kuwapokea na kuwapa mkataba wachezaji wanaodaiwa kutemwa katika kikosi cha Simba kutokana na utovu wa nidhamu.
Hivi karibuni kumekuwapo na tetesi za wachezaji hao wa Simba ambao ni Juma Nyoso, Ramadhan Chombo ‘Redondo,’ pamoja na Amir Maftah kuhusishwa kutaka kujiunga na Ashanti United kwa ajili ya kuitumikia katika michuano ya Ligi Kuu msimu ujao.
Katibu Mkuu wa Ashanti United, Abubakari Siyas alisema jana kuwa, timu hiyo siyo kituo cha tiba kwa watovu wa nidhamu hivyo wachezaji hao hawana nafasi ya kuitumikia klabu hiyo. Alisema sera ya Ashanti United siku zote ni kutumia wachezaji wa ridhaa wenye nidhamu na moyo wa kujitolea