Mabao
ya City yamefungwa na Samir Nasri dakika ya 39 na Nahodha Vincent
Kompany dakika ya 49. Liverpool imetoka nyuma na kushinda 2-1 dhidi ya
Newcastle United. Skrtel alijifunga dakika ya 20 kuipa Newcastle bao la
kuongoza, lakini Daniel Agger akaisawazishia Liverpool dakika ya 63
kabla ya Daniel Sturridge kufunga la ushindi dakika ya 65.
Chelsea
imemaliza katika nafasi ya tatu baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Cardiff
City mabao yakw yakitiwa kimiani na Schurrle dakika ya 72 na Torres
dakika ya 75, huku bao la wapinzani wao likifungwa na Bellamy dakika ya
15.
Arsenal imemaiza katika nafasi ya nne kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Norwich City, mabao ya Ramsey dakika ya 53 na Jenkinson dakika ya 62. Everton iliyoifunga 2-0 Hull City imemaliza katika nafasi ya tano, wakati Tottenham Hotspur imemaliza ya sita baada ya kuifunga 3-0 Aston Villa na Manchester United iliyotoa sare ya 1-1 na Southampton imemaliza ya saba.
Kama ilivyo ada, bingwa na timu tatu za chini yake watacheza Ligi ya Mabingwa, wakati wa tano wa sita watakwenda Europa League.
| Samir Nasri akishangilia bao lake |
