come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

Mourinho asaka nyota sita

Jose Maurinho  

LONDON, ENGLAND
JOSE Mourinho ambaye atawasili Chelsea Julai Mosi,  amedaiwa kuanza kusaka majina sita ya kuyasajili kwenye dirisha la majira ya joto.
Habari zinasema kocha huyo ana orodha ya mabeki wawili, viungo wawili na washambuliaji wawili.
Mourinho ataondoka rasmi Real Madrid Juni 2 na kuna habari kuwa huenda akatambulishwa kabla ya Julai. Licha ya kuwa na majina hayo, kocha huyo pia amewataka wachezaji wakubwa wasaini nyongeza ya mwaka mmoja kama walivyotakiwa kufanya na viongozi wa juu.
Kocha huyo amebainisha kuwa timu nzuri ni ile yenye mchanganyiko wa wakongwe na vijana.
Imefahamika kuwa baadhi ya majina makubwa kwenye orodha ya kocha huyo ni Radamel Falcao wa Atletico Madrid, kiungo wa Malaga, Isco, nyota wa Everton, Marouane Fellaini na beki wa Porto, Eliquim Mangala. 
Lakini viongozi wa sasa wa Chelsea wapo katika hatua nzuri ya kumsajili mshambuliaji wa Bayern Leverkusen, Andre Schurrle na Mourinho amewataka wamrudishe kipa, Thibaut Courtois ambaye yupo Atletico kwa mkopo wa muda mrefu.