come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

NGASSA ANAVYOZIUMIZA KICHWA SIMBA NA EL MEREIKHY


LAZIMA tuamini kwamba aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa amejiunga na Yanga na ataichezea timu hiyo michuano yoyote itakayoshiriki kuanzia sasa.
Ngassa amejiunga na Yanga huku kukiwa na vitimbi kadhaa vilivyotokea tangu anaondoka katika timu hiyo miaka michache iliyopita, wakati huo Yanga ilikuwa chini ya Mwenyekiti, Iman Madega.
Winga huyo aliondoka Yanga na kujiunga na Azam FC katika usajili ambao haukutarajiwa na wengi kutokana na mapenzi ya Ngassa kwa Yanga, bila shaka fedha iliongea. Azam ililipa zaidi ya Sh. 90 milioni ili kumnasa mchezaji huyo.
Mwaka jana katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, akiwa anaichezea Azam, Ngassa baada ya kuifungia bao muhimu timu hiyo katika nusu fainali, alikwenda kwenye kibendera cha kona na kukibusu. Kibendera hicho kina rangi ya kijani na njano, rangi hizo zinatumiwa na Yanga.
Hiyo ilionekana kama ishara ya kuitukuza Yanga na kuidharau Azam timu inamlipa mshahara na posho nyingine, kwa kifupi ni mwajiri wake. Azam haikupendezwa na hali hiyo, kabla ya kuanza kwa msimu huu ikatangaza kumtoa kwa mkopo kwa Simba.
Wakati Azam inatangaza kumtoa kwa mkopo au kumuuza Ngassa, nilijua fika kwamba Yanga inaweza kutia mkono wake hivyo ikatazama mazingira ya kumkwamisha kurejea katika klabu yake na kuhakikisha anakwenda Simba.
Alipokuwa Simba, Ngassa alipata ‘deal’ la kujiunga na klabu ya El Merreikh ya Sudan, viongozi wa Simba walizungumza na El Merreikh bila ya kupata ridhaa ya Ngassa. Mwisho wake mchezaji alikataa kujiungana timu hiyo ya Sudan.
Azam ambayo nayo ingefaidika kama Ngassa angejiunga na El Merreikh, ni wazi haikupendezwa na hali hiyo ya Ngassa kukataa kuiunga na klabu hiyo. Mkakati ukapangwa.
Lakini wakati haya yakitokea siku za nyuma hebu tutazame namna Ngassa alivyosajiliwa na Yanga huku kukiwa na mambo kadhaa ya kushangaza;
NGASSA HAJAPIMWA AFYA

Kama ilivyo kawaida ya timu nyingi za Tanzania, safari hii Ngassa amesajiliwa na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili bila ya kupimwa afya…!
Jambo hili la wachezaji kusajiliwa bila kupimwa afya sasa linaonekana la kawaida ambalo klabu zimerithi utaratibu huo toka zamani, Dunia imebadilika lakini viongozi wengi wa soka hapa nchini hawatazami hili.
Kwa mfano Ngassa anaweza kuwa na matatizo ya afya katika viungo vyake vya mwili ambavyo baadaye anaweza kuigharimu klabu kumgharamia matibabu kwa mfano matatizo ya goti.
Matibabu hayo yanaweza kuigharimu klabu kiasi kikubwa cha fedha ambacho kingeweza kufidiwa wakati wa usajili wake.
FEDHA ZA EL MERREIKH ZAMPONZA
Kama inavyodaiwa kwamba, Ngassa amesaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuitumikia Simba, baada ya deal la kumpeleka El Merreikh kushindikana, Simba na Azam ziliamua kupeleka mkataba huo wa Simba kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ili kuusajili ili Ngassa asiwe na uamuzi mwingine atakapoamua timu ya kujiunga nayo mkataba wake utakapoisha Azam.  
Lengo la Azam na Simba lilikuwa ni kuona Ngassa hajiungi na Yanga na anaichezea Simba msimu ujao pia, HATA KAMA BILA RIDHAA YAKE.
Kwa kuwa Ngassa anafahamu anachofanya na anaheshimu maamuzi yake, aliamua kusaini kuichezea Yanga ili acheze soka kwa amani zaidi.
Usajili wa Ngassa kwa Simba (kama kweli alisaini) ulikuwa wa kama ‘kishika uchumba’ ili awe na uhakika na ahadi ya kusajiliwa na klabu hiyo, hivyo baadaye angeweza kuwa na maamuzi mengine kama alivyofanya sasa.
NGASSA NI HALALI YANGA
Kama kweli TFF itafuata hatua kwa hatua katika kile kinachoitwa mkataba wake na Simba, Ngassa ataichezea Yanga msimu ujao, kwani kuna vitu vingi vilifanyika katika mkataba huo bila ridhaa ya mchezaji.
Jambo hili linaweza kuwa kama la usajili wa Kelvin Yondani na Mbuyu Twite.