![]() |
|
|
|
Louis Van Gaal amemtetea Marouane Fellaini dhidi
ya madai kwamba kiungo huyo wa kati wa Manchester United kutoka Ubelgiji
alimtemea mate Sergio Aguero wa Manchester City wakati wa debi
iliyochezewa Etihad Jumapili.
Mitandao ya kijamii iliwaka, mjadala mkuu ukiwa iwapo video ya kisa kilichotokea kipindi cha kwanza ambapo Fellaini alisimama kando ya Aguero aliyekuwa ameanguka, na kumshutumu kwa kujiangusha, pia ilionyesha akimtemea mate straika huyo wa Argentina, aliyeshindia City 1-0.
Hata hivyo meneja wa United Van Gaal alisisitiza Fellaini si mtu wa “kutemeana mate” na wanaotazama video hiyo wameona tu ishara za hasira kutoka wka mchezaji huyo.
Fellaini bila shaka alikuwa ameghadhabishwa na kuanguka kwa Aguero eneo la hatari, na alimgeukia na kumkaripia baada ya refa Michael Oliver kukataa ombi la straika huyo la kutaka penalti.
"Nimesikia kwamba hilo linajadiliwa mitandao ya kijamii lakini tayari iwapo (Fellaini) anasema kwa sauti na wakati ukisema kwa sauti, kuna – mnayaitaje, mate? – pamoja. Sidhani yeye ni mtu wa kutemeana mate,” akasema Van Gaal.
Mitandao ya kijamii iliwaka, mjadala mkuu ukiwa iwapo video ya kisa kilichotokea kipindi cha kwanza ambapo Fellaini alisimama kando ya Aguero aliyekuwa ameanguka, na kumshutumu kwa kujiangusha, pia ilionyesha akimtemea mate straika huyo wa Argentina, aliyeshindia City 1-0.
Hata hivyo meneja wa United Van Gaal alisisitiza Fellaini si mtu wa “kutemeana mate” na wanaotazama video hiyo wameona tu ishara za hasira kutoka wka mchezaji huyo.
Fellaini bila shaka alikuwa ameghadhabishwa na kuanguka kwa Aguero eneo la hatari, na alimgeukia na kumkaripia baada ya refa Michael Oliver kukataa ombi la straika huyo la kutaka penalti.
"Nimesikia kwamba hilo linajadiliwa mitandao ya kijamii lakini tayari iwapo (Fellaini) anasema kwa sauti na wakati ukisema kwa sauti, kuna – mnayaitaje, mate? – pamoja. Sidhani yeye ni mtu wa kutemeana mate,” akasema Van Gaal.
