KAMA kuna timu iliyotaabika kwenye nafasi ya ulinzi ni Simba. 
Timu hiyo kwa karibu mwaka mmoja sasa imekuwa ikipepesuka hasa baada ya 
kuondoka mchezaji wao Kelvin Yondani aliyejiunga na Yanga.
Wachezaji ambao wamekuwa wakisajili kwenye nafasi 
hiyo wameshindwa kuhimili vishindo na kufanya ukuta wa Simba kuyumba 
kila mara na kufanya timu hiyo ishindwe kushindana kisawa sawa.
Lawama kubwa zimekuwa zikielekezwa kwenye kamati 
ya usajili kwa maelezo kuwa imekuwa ikifanya mambo kwa mazoea kuliko 
utaalamu katika kutafuta wachezaji, hususani wa kuziba nafasi hiyo ya 
ulinzi.
Tayari imewajaribu mabeki saba kucheza nafasi hiyo
 lakini wamechemka na kujikuta wakitupiwa virago ingawa wengine waliamua
 hata kuvunja mikataba yao kuhamia klabu nyingine.
Lino Musombo (Congo)
SIMBA ilidai imepata mtu sahihi kumaliza tatizo la
 kuondoka kwa beki wake wa kati, Kelvin Yondani ingawa baada ya muda 
mfupi alitupiwa virago.
Lino alikuwa ameenda hewani vizuri na mwili mkubwa
 ambao unamwezesha kukabiliana na kashikashi zozote uwanjani. Ingawa 
Simba hawakuwa na subira ya kumvumilia na kuamua  kumtupia virago.
Simba walifanya uamuzi wa haraka kwa lugha rahisi 
walikurupuka katika kufanya uamuzi wa kumtimua beki huyo kwani kadri 
muda ulivyosonga alizidi kuimarika kiuchezaji.
 (Kenya)
MKENYA ambaye ameenda vizuri hewani na umbo kubwa.
 Ni wazi umbo lake linawatisha mastraika kumpita ingawa kuna jambo pekee
 ambalo limemfanya beki huyo wa kati aliyewika na timu ya Taifa ya Kenya
 ‘Harambee Stars’ aonekane kuwa hawezi kuendelea kuitumikia Simba na 
kutupiwa virago.
Kwa mujibu wa benchi la ufundi la Simba lilidai 
kuwa sababu kubwa ya kumtema kitasa huyo ni kushindwa kuendana na kasi 
ya baadhi ya washambuliaji wa timu za Ligi Kuu Bara.
Ochieng aliuachia mwili wake na kumfanya awe 
mzito. Aliyekuwa Kocha wa Simba, Mserbia Milovan Cirkovic alimtaka beki 
huyo kufanya mazoezi magumu kwa ajili ya kukata mwili huo.
 
