Lionel Messi.
Jaji wa mahakama hiyo, Anju Deb Rani, alisema watu hao watapanda kizimbani Septemba 17.
Messi ambaye ni Mwanasoka Bora wa Dunia mara nne, 
pamoja na baba yake huyo, Jorge Horacio, watafika mahakamani ikiwa ni 
utaratibu wa kawaida wa mahakama kabla ya kuanza uchunguzi rasmi. 
Jaji alisema malalamiko ya ukwepaji kodi 
yaliwafikia na wamechukua hatua ya kuwaita watu hao mahakamani ikiwa ni 
utaratibu wa kawaida wa mahakama.  Alisema: “Baada ya tukio hilo, 
uchunguzi wa kina utafanyika kuona kama jambo hilo ni la kweli au la.”
Juni 12 Messi alidaiwa kukwepa kodi kwa miaka mitatu kuanzia 2007 mpaka 2009.
Kama wakipatikana na hatia, wawili hao watatoa 
fidia ya asilimia 150 ya kodi waliyokwepa au kifungo jela cha kati ya 
miaka miwili mpaka sita.
 
