come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

YANGA KUIKACHA MICHUANO YA KAGAME!

Serikali imesema ina hofu ya usalama wa wachezaji wa timu za Tanzania zitakazoshiriki Kombe la Kagame la klabu bingwa ya soka Afrika Mashariki na Kati mwezi ujao nchini Sudan, kutokana na kufayika katika jimbo la Darfur.

Mabingwa watetezi Yanga, Simba na Super Falcon ya Zanzibar zinataraji kushiriki katika michuano hiyo ya mwezi ujao ambayo imepangwa kucheza katika vituo viwili vya Alfashery, mji wa Darfur kaskazini, na Kadugli.
Akijibu hoja za wabunge walizozitoa katika kuchangia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa jana Bungeni hapa, Bernard Membe alisema:
Hali ya usalama ni ya wasiwasi (Darfur) kwa sababu watu wanaokwenda huko wanapokewa na vikosi vya magari yasiyoingia risasi na huvishwa nguo ambazo hazipenyezi risasi.
“Wageni wote wanaokwenda Darfur huwa wanapokelewa na magari ambayo ni bullet proof (yenye kuzuia risasi) na wanapewa t-shirt zenye bullet proof,” alisema na kuongeza:
"Nimeshangaa mipango hii ya kupeleka wanamichezo huko bila maandalizi makubwa na si kwa upande wetu (bali) wale walioandaa michezo hii Darfur.”
Shirikisho la soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) ndilo lililopanga vituo viwili hivyo vya nchini Sudan kwa ajili ya michuano hiyo ya kila mwaka.
Katika Kombe la Kagame, Yanga imepangwa katika Kundi C pamoja na timu za Express (Uganda), Ports (Djibout) na Vital’O (Burundi).
Simba ipo kwenye kundi A pamoja na timu za El-Merrekh (Sudan), APR (Rwanda) na Elman (Somalia).
Kundi B lina timu za Al-Hillal (Sudan), Tusker FC (Kenya), Al Nasri (Sudan Kusini), Falcon (Zanzibar) na Al Ahly Shandy (Sudan).
Mechi za Kundi A na C ndizo zitachezwa Alfashery.
Membe alisema anashangaa busara iliyotumiwa na CECAFA kuchagua jimbo la Darfur kuwa sehemu ya kufanyia mashindano hayo kwa sababu "usalama wa vijana utakuwa katika mashaka."
"Kwanini wamechagua kuwa sehemu mojawapo ya kuchezea mechi?”