come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

MWILI WA NGWAIR KUWASILI WIKI IJAYO JUMANNE

Dar es Salaam. Mwili wa msanii wa muziki wa Hip Hop, Albert Mangwea maarufu kama Ngweiar (31), uliotarajiwa kuwasili leo huenda isiwe hivyo kutokana na kutokamilika kwa baadhi ya mambo ikiwemo ripoti ya daktari nchini Afrika Kusini.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Wasanii nchini, Addo Novemba aliliambia gazeti hili jana kuwa wanaendelea kuwasiliana na watu walioko Afrika Kusini ili kujua ni lini utaletwa.
Awali, mwili wa Ngweair aliyefariki Afrika Kusini alikokwenda kwa shughuli za muziki, ulitarajiwa kuletwa jana, lakini ilishindikana kufuatia Watanzania wanaoishi nchini humo nao kutaka kupata fursa ya kuuaga kabla ya kusafirishwa leo.
Novemba alisema ratiba ya awali ilionyesha kuwa shughuli ya kuuaga mwili wa Mangwea ingeanza saa mbili asubuhi mpaka saa sita mchana Jumatatu, kabla ya kusafirishwa kwenda mkoani Morogoro kwa mazishi.
Wakati huohuo, Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo imetoa pole kwa wasanii na wadau mbalimbali wa tasnia ya muziki kufuatia kifo cha msanii huyo.
“Kifo cha Albert Mangwea ni pigo kubwa kwa fani ya muziki hapa nchini, na pia kimataifa, ni kutokana na umahiri wake katika fani hiyo ya muziki wa kizazi kipya hususan aina yake ya uimbaji ya “Free Style” alikonga mioyo ya wapenzi wake hasa vijana ndani na nje ya nchi.” ilisema taarifa hiyo ya Wizara iliyosainiwa na Waziri Fenella Mukangara.
“Mangwea atakumbukwa na wadau wa muziki kwa kipaji na juhudi zake za kukuza muziki hapa nchini.Serikali inawapa pole ndugu na jamaa.”