come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

YANGA YAIPIGA MWELEKA SIMBA, KUJENGA UWANJA WA KISASA BUNJU

Upo uwezekano mkubwa uwanja wa kisasa wa klabu ya Yanga ukajengwa mahali tofauti na Kaunda kutokana na udogo wa eneo la Jangwani, imeelezwa.

Akizungumza jana, mmoja wa wajumbe wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo ambaye hakutaka jina lake kutajwa gazetini kwa sababu si msemaji wa masuala ya uwanja alisema:
Kwa kuangalia michoro ya uwanja mpya na mahali ambapo klabu inakusudia kujenga uwanja huo, ni vigumu uwanja ukawa kwenye eneo la Kaunda.
Alisema kutokana na kuwapo kwa ugumu huo, uongozi unaendelea kuangalia cha kufanya ili kufanikisha ujenzi huo, ambao umekuwa ukiahidiwa na awamu mbalimbali za utawala wa Yanga kwa miaka 20 sasa.
Mahasimu wa Yanga kwenye ligi kuu ya Bara, Simba, wanadai kuwa katika mchakato wa kujenga uwanja wake wa kisasa katika kitongoji cha Bunju, km 40 kutoka klabuni Msimbazi.
Uwanja wa Kaunda ulijengwa na waasisi wa klabu hiyo mwanzoni mwa miaka ya 1970 lakini kwa sasa umezungukwa na makazi ya watu licha ya kuwa kwenye bonde la mto Msimbazi.
Ingawa uongozi wa Yanga ulikaririwa na gazeti moja mapema wiki hii ukidai umetuma maombi ya kunyakua nyumba hizo Wizara ya Ardhi, jambo hilo haliwezekani.
Kisheria mikono ya serikali imefungwa katika kutwaa makazi binafsi hayo kwa sababu uwanja huo si kwa ajili ya maslahi ya umma hivyo Yanga inatakiwa kushawishi majirani zake hao kuuza maeneo yao hayo kwake.
"Ukitazama michoro ni wazi pale hapatoshi lakini bado tunatafutwa njia nyingine za kuona ujenzi huo unafanikiwaje," alisema mjumbe huyo.
Alipoulizwa kama wanaweza kutafuta eneo lingine kwa ajili ya ujenzi huo, mjumbe huyo alisema hana uhakika lakini ikibidi watafanya hivyo.
"Nafikiri ukimtafuta makamu mwenyekiti (Clement Sanga) anaweza akakufafanulia kwa undani zaidi... mimi si msemaji.
"Lakini kikubwa ni klabu kuwa na uwanja wake hivyo kama pale patashindikana nafikiri kutakuwa na busara ya kutafuta eneo lingine."
Simu ya mkononi ya Sanga haikuwa ikipatikana alipotafutwa jana, hata hivyo.
Yanga imekabidhiwa michoro ya uwanja wenye kuketisha watazamaji 30,000 inaokusudia kujenga na mkandarasi kampuni ya Beijing Construction ambayo moja ya kazi zake nchini ni Uwanja wa Taifa wenye kuingiza watazamani chini kidogo ya 60,000.