come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

MADA MAUGO ASHANGAA MASHALI KUINGIA KWENYE NDONDI BADALA YA UPISHI

Bondia namba tatu hapa nchini kwenye uzani wa Ssuper middle, Mada ‘King’ Maugo (Pichani) amebainisha kuwa mpinzani wake Thomas Mashali hampi homa hata kidogo.

“Mashali hanipi mawazo hata kidogo, tena kwa kumshauri kwa ngumi anazocheza bora akaombe kazi ya kupika chapati au mandazi hotelini,” alisema Maugo jana kwenye mahojiano na Mtandao huu
Maugo na Mashali watapanda ulingoni Agosti 30 kuzichapa kuwania ubingwa wa WBF Afrika kwenye uzani wa Ssuper middle kg 76 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam ambapo pia Francis Cheka atacheza na Derick Findley wa Marekani huku Alphonce Mchumiatumbo atazipacha na De Andre McCole wa Marekani katika uzani wa juu pambano la raundi 10.
“Sina presha ya mazoezi hivi sasa kwa ajili ya Mashali, ni bondia mdogo mno kwangu yule namfanyia mazoezi ya siku tano tu yanamtosha, hanipi homa hata kidogo, muacheni aropoke anavyotaka mimi sasa hivi sitaki kuongea sana nitaonyesha vitendo ulingoni,” alitamba Maugo.
Bondia huyo aliyevunja rekodi ya kuwa na maneno mengi kwa mabondia wa Tanzania aliendelea kubainisha kuwa mpinzani wake huyo siku hiyo atamtambua vizuri yeye ni bondia wa aina gani.
“Alipocheza na Cheka akawa anadondoka dondoka hajakoma sasa namvunja mbavu, anajifanya anafanya mazoezi viwanja vya chuo kwa ngumi gani anazocheza sana akaombe kazi ya kupika chapati hotelini,” aliponda bondia huyo.
Akizungumzia pambano lake la Russia dhidi ya Movsur Yusupovka litakalofanyika Julai 27 kwenye ukumbi wa Trade &Intertainment uliopo mjini Kaspiysk, Maugo alisema yuko fiti na kusisitiza anategemea matokeo mazuri.
“Naondoka Jumanne ijayo nchini ambapo nitakwenda moja kwa moja Russia tayari kwa pambano hilo,” alisema Maugo na kuongeza kuwa atakaporejea atapumzika kwa muda kabla ya kufanya mazoezi ya siku tano.