come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

MICHAEL ESSIEN AFUNGA NDOA GHANA

 
BAADA ya uvumi wa muda mrefu kuhusu uhusiano wake wa kimapenzi, inasemekana staa wa Chelsea na timu ya taifa ya Ghana, Michael Essien, amefunga ndoa ya kimya kimya na mrembo, Akosua Puni, ambaye sasa anajitambulisha kwa jina la ‘Mrs. Akosua Puni-Essien’.
Mrembo huyo anamfanyia Essien kazi zake za uhusiano ya jamii akiwa mkuu wa mfuko wa Essien ujulikanao ‘kama Michael Essien Foundation’unaolenga kuimarisha huduma za kijamii nchini Ghana.
Lakini baada ya muda wa kazi, kumbe wawili hao ni wapenzi wazuri na baada ya kuwa wapenzi wa muda mrefu kwa uhusiano wa kimya kimya, Essien ameamua kuchukua mzigo jumla.
Akosua ameonekana katika Jiji la Accra akirandaranda na pete ya ndoa ya Essien kitendo ambacho kinaashiria kwamba wawili hao wamefunga ndoa.
Hivi karibuni, wawili hao walionekana wakila raha katika hoteli ya Imperial Peking jijini Accra ambako Essien alikuwa na kalamu maalumu ya chakula cha jioni kwa ajili ya kuendesha mfuko wa hisani kwa ajili ya kuchangia upatikanaji wa maji kijijini kwao.
Kabla ya hafla hiyo, jioni yake Essien aliandaa mechi iliyowakutanisha mastaa kama Florent Malouda, Michael Ballack, Jay Jay Okocha na wengine kwa ajili ya kuchangia mradi wake huo.
Imefahamika kuwa wakati uvumi ulipokuwa umeenea mwaka mmoja uliopita kuwa Essien alikuwa amefunga ndoa na mwigizaji maarufu wa Ghana, Nadia Buari katika sehemu moja ya siri jijini London, kumbe aliyekuwa amefunga ndoa na Essien ni Akosua.
Imethibitika kwamba Essien na Akosua ni wanandoa rasmi ambao wana watoto wawili wanaoishi nao Uingereza, jambo ambalo limezua mjadala mkubwa ni kwa nini Essien aliamua kumtema Nadia ambaye ni mrembo maarufu zaidi nchini Ghana?
Mjadala mkubwa uliopamba moto katika vyombo vya habari vya Ghana ni ule ambao unajaribu kuwalinganisha Nadia na Akosua. Maswali yanaulizwa kuhusu yupi kati yao ana mwonekano mzuri zaidi kwa nje. Lakini pia maswali yamekuwa yakiulizwa kuhusu yupi kati yao ana tabia njema za ndani ambazo zinaweza kumfanya awe mke wa mwanasoka maarufu wa hadhi ya Essien ambaye anachukuliwa kuwa shujaa nchini kwao Ghana.
Ni wazi kwamba chaguo la Essien kwa Akosua dhidi ya Nadia linamaanisha kwamba Essien ameangalia tabia zaidi ndani na si za nje.
Nadia ambaye ni mtoto wa mwanamuziki maarufu wa zamani wa Ghana, Sidiku Buari,anatajwa kuwa mrembo zaidi kuliko Akosua.