come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

NEYMAR 1-0 MESSI...NYOTA WA BRAZIL AMGARAGAZA MWANASOKA BORA WA DUNIA PERU

Shake on it: Argentina's Lionel Messi (right) and Brazil's NeymarMBRAZIL Neymar na Muargentina, Lionel Messi wataunda pamoja safu kali ya ushambuliaji ya Barcelona msimu ujao, lakini walikuwa timu tofauti leo katika mechi ya Hisani nchini Peru.

Nyota hao wa Amerika Kusini, waliungana na wakali kama Daniel Alves, Ezequiel Lavezzi, Javier Mascherano na Eric Abidal kwa mechi hiyo baina ya Messi na marafiki zake dhidi ya wachezaji wengine duniani.
Karibu sana: Lionel Messi (kulia) na Neymar
Argentina's Lionel Messi (R) and Brazil's Neymar embrace each other before an exhibition match
Barca boys: But Neymar and Messi were on opposite sides for charity match
Vijana wa Barca: Lakini Neymar na Messi walikuwa timu tofauti katika mechi hiyo ya hisani
Ilikuwa mara ya kwanza wanakutana uwanjani tangu gwiji wa Barca, Johan Cruyff ashauri mshindi mara nne wa Balon D'or, Messi auzwe kumuachia nafasi mchezaji mwenzake mpya aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 50.
Na Neymar alimgaragaza Messi, ambao wote walivaa jezi namba 10 katika mechi hiyo, kwa kufunga bao la umbali wa mita 45.
Na baadaye akamnyanyasa beki wa Malaga na Uruguay, Diego Lugano.
Lakini Messi ndiye aliyeibuka kifua mbele mwishowe kwa timu yake kushinda 8-5. 
Fedha zote zitakazopatikana katika mchezo huo, zitakwenda kwenye mfuko wa kujenga mustakabali mzuri wa maisha kwa watoto kimataifa.
On the ball: Neymar, left, controls takes on Argentina's Javier Mascherano, right,
Mwenye mpira: Neymar, kushoto, akimtoka Muargentina, Javier Mascherano, kulia,
Front man: Lionel Messi, left, organised the charity match in Peru
Mtu wa mbele: Lionel Messi, kushoto, ameandaa mechi ya Hisani Peru
Friends reunited: Messi withDaniel Alves, Ezequiel Lavezzi and Eric Abidal
Marafiki wameungana: Messi na Daniel Alves, Ezequiel Lavezzi na Eric Abidal