
Mshambuliaji wa Liverpool akikabiliana na mlinda mlango wa Arsenal Wojciech Szcesny
Liverpool imewadhalilisha
waliokuwa vinara wa ligi kuu ya England, Arsenal baada ya kuwaangushia
kipigo kikali cha magoli 5-1 katika uwanja wa Anfield.
Skirtel akipachika magoli yake katika dakika ya 1 na 10, Sterling akiongezea machungu kwa Arsenal kwa kupachika goli la tatu katika dakika ya 16 na Sturridge akihitimisha karamu ya magoli ya Liverpool kwa dakika 45 za kwanza za mchezo kwa kupachika goli katika dakika ya 20.

Wachezaji wa Arsenal
Matokeo hayo yalibadilisha msimamo wa ligi hiyo. Chelsea baada ya ushindi wao wa mabao 3-0 dhidi ya Newcastle, kuliwapandisha kileleni mwa ligi hiyo, ikiwa imejikusanyia pointi 56, Arsenal ikiteremka na kukalia nafasi ya pili ikiwa na pointi 55, Manchester City nayo imeteremka na kushika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 54 baada ya kubanwa mbavu na Norwich ambao walitoka nao sare ya kutofungana.
Liverpool kwa sasa imejikusanyia pointi 50 na kutulia nafasi ya nne baada ya michezo 25 kwa timu zote hapo juu.
Manchester United leo inakipiga na Fulham inayozibeba timu zote 19, ikiwa ni ya 20. Pia mchezo mwingine mkali unatarajiwa kuwa kati ya Tottenham yenye pointi 44 dhidi ya Everton yenye pointi 45 ikiwa nafasi ya tano.
Everton ikishinda itabakia nafasi yake ya tano kwani itakuwa na pointi 48, lakini Tottenham ikishinda basi itachukua nafasi ya sasa ya Everton kwa kufikisha pointi 47. Ushindi wa Manchester United dhidi ya Fulham hautabadili nafasi yake ya saba, mbali na kujiongezea pointi. Kwa sasa ina pointi 40.