come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

UHURU, NYOSSO, BOBAN WAMKUNA KOCHA COASTAL UNION

Kocha wa Coastal Union ya Tanga, Hemed Morocco amesema anafurahishwa na viwango vinavyoonyeshwa na wachezaji wake wakiwamo nyota wa Simba waliohamia klabu hiyo.

Union iliyo kambini Raskazoni, inaendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga ikijiandaa na Ligi Kuu msimu ujao unayotarajiwa kuanza mwezi ujao.
Morocco aliuambia mtandao huu jana kuwa, tangu aanze mazoezi vijana wake wameonyesha kujituma na kufanya mazoezi kwa bidii.
“Nashukuru mazoezi yanakwenda vizuri, mpaka sasa wachezaji wote wameripoti kambini, ushindani umeongezeka kama mnavyojua kutokana na kuwepo kwa wachezaji wenye uwezo,” alisema Morocco. Alisema uwepo wa wachezaji wapya ndani ya kikosi chake kumeongeza ushindani mkubwa miongoni mwa wachezaji. Baadhi ya wachezaji wapya na wenye uzoefu ni Haruna Moshi Boban, Uhuru Seleman na Juma Nyosso waliojiunga kutoka Simba na Azam FC.