come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

#TAARIFA : TMA YATOA TAHADHARI KUEPUKA MADHARA YA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA

Na mwandishi wetu Dar es Salaam.

KUFUATIA mvua zinazoendelea kunyesha karibu katika kila kona ya nchi mamlaka ya hali ya hewa Tanzania TMA imetoa hadhari kwa wananchi wanaoishi katika maeneo hatarishi kuchukua hadhari ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hali ya hewa nchini Agness Kijazi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Amesema wananchi mvua zilitarajiwa kunyesha tarehe 13 hadi tarehe jumamosi tarehe 16 mwezi huu.

Ameongeza kuwa wananchi wanatakiwa kuchukukua hadhari kubwa kwani mvua zinatarajiwa kunyesha kwa asilimia 70 na zitakuwa na kimbunga aina ya Fantana katika bahari ya Hindi.

Amesema Mkoa inayotarajiwa kuwa na mvua nyingi ni pamoja na Dar es salaam, Tanga, Morogoro, Pwani na Visiwa vya Unguja.