come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

#TANZIA: PAPA WEMBA AAGA DUNIA

Na Elias John.

Mwanamuziki wa miondoko ya soukos rhumba mwenye asili ya DRC Kongo Jules shungu pene wembadio kikumba almaarufu Papa Wemba amefariki dunia leo huko nchini Ivory Coast.

Wemba aliyewahi kuhudumu bendi za Zaiko langalanga na viva la muziki amekutwa na umauti huo akiwa jukwaani ambapo ghafla alianza kutetemeka na kuanguka na kupoteza uhai papo hapo.

Papa Wemba aliwahi kutamba na vibao kama Show me the way na nyinginezo na kwamba atakumbukwa kwa sauti yake nyororo ya kumtoa nyoka pangoni.

Wemba amezaliwa nchini Kongo katika kitongoji cha lubefu senkulu tarehe 14 june 1949 na amefariki dunia leo tarehe 24 April 2016 nchini Ivory Coast.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Papa Wemba mahali pema peponi amina.

Pichani mwanamuziki Papa Wemba enzi za uhai wake.