come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

MAN UNITED AIBU TUPU, MOYES AJIPA MOYO.

Ushindi wa vinara wa ligi kuu ya England Arsenal dhidi ya wapinzani wao wa jadi wa jiji la London,Tottenham, Jumamosi kunawapambanisha na Coventry City walio daraja la kwanza katika mzunguko wa nne wa kombe la FA.

Katika mchezo huo Arsenal iliichakaza Tottenham magoli 2-0.
Arsenal, The Gunners, ambao waliondolewa na Blackburn Rovers katika mzunguko wa tano wa mashindano kama hayo mwaka 2013, itapenda kufanya vyema ili kutwaa kombe la FA ambalo kwa mara ya mwisho ililitwaa mwaka 2005.


Nayo Swansea, kwa kuichapa Manchester United 2-1 katika uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford, Jumapili ni fursa ya kupambana na moja wapo ya timu za Birmingham City, Bristol Rovers ya daraja la pili au Crawley ya

daraja la kwanza- huku mechi ya Crawley ya mzunguko wa pili iliyoahirishwa ikiwa bado kuchezwa.

Mabingwa watetezi wa kombe hilo Wigan wataikaribisha Crystal Palace iwapo wataifunga MK Dons katika mechi yao ya marudiano baada ya timu hizo kwenda sare ya 3-3 Jumamosi.

Ratiba ya Kombe la FA mzunguko wa nne:

Sunderland kupambana na Kidderminster au Peterborough
Bolton kupambana na Cardiff
Southampton itapambana na Yeovil
Huddersfield itakabiliana na Charlton au Oxford
Port Vale au Plymouth itachuana na Brighton
Nottingham Forest itamenyana na Ipswich au Preston

Southend na Hull

Rochdale dhidi ya Macclesfield au Sheffield Wednesday
Arsenal uso kwa uso na Coventry
Stevenage itaonyeshana kazi na Everton
Wigan au MK Dons itanyukana na Crystal Palace

Chelsea dhidi ya Stoke
Blackburn au Manchester City itapepetana na Bristol City au Watford
Bournemouth au Burton kivumbi dhidi ya Liverpool
Birmingham, Bristol Rovers au Crawley itacheza dhidi ya Swansea
Sheffield United itapambana na Norwich au Fulham

Mechi hizo za mzunguko wa nne zitachezwa kati ya tarehe 25 na 26 mwezi Januari, 2014.