come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

#TAARIFA: NDANDA KOSOVO KUZIKWA JUMATANO.

Na mwandishi wetu.

Mwanamuziki nguli wa miondoko ya dansi mwenye asili ya Kongo Ndanda Kosovo almaarufu kichaa, anatarajiwa kuzikwa siku ya jumatano katika makaburi ya kinondoni jijini Dar es Salaam.

Marehemu Ndanda amefariki dunia siku jumamosi ya wiki iliyopita katika hospitali ya Taifa jijini Dar es Salaam alikolazwa kwa ajili ya matibabu ya vidonda vya tumbo.

Kosovo amewahi kutamba na kibao chake Binadamu ambacho amekifyatua akiwa na kundi lake la Fm academia wajela jela gwaa.

Ndanda ni miongoni mwa wana
muziki waanzilishi wa kundi la Fm academia,  na atakumbukwa mashabiki wake kutokana na staili yake ya uimbaji na mbwembwe zake jukwaani.