come

come
Tuletee habari za kijamii, michezo na burudani, email kabumbu1935@gmail.com

#VITUKO: NAPENDA KUOGA BILA SABUNI: IDRIS


Na Mwandishi wetu

KINARA kunako jumba la Big Brother Africa (BBA) mwaka 2015-2016 Comedian Idris Sultan amesema yeye pamoja umaarufu alionao na mkwanja wa maana alloupata baada ya kushinda BBA Kwake kuoga bila sabuni ni jambo la kawaida.

Idris ameyasema hayo alipokuwa akihojiwa na mtangazaji mwenye jina kuwa hapa town Salama Jabri katika kipindi cha mkasi kinachorushwa na EATV.

Idris ambaye ana kipaji kikubwa cha uchekeshaji amesema yeye kufikia hapa alipo sasa ni juhudi za watanzania na wananchi wa nchi nyingine Duniani kwa kumpigia kura za kutosha zilizomsaidia yeye kuibuka mshindi katika mashindano hayo.

Ameongeza kuwa kwa sasa amamalizia mchakato wa kuandaa filamu yake ya vichekesho pamoja vipindi viwili vya runinga yaani (TV SHOWS) na kuwaomba mashabiki wake kuendelea kumuunga mnono.